This is an automatically generated PDF version of the online resource tanzania.mom-gmr.org/en/ retrieved on 2024/04/19 at 00:27
Global Media Registry (GMR) & Media Council of Tanzania - all rights reserved, published under Creative Commons Attribution-NoDerivatives 4.0 International License.
Media Council of Tanzania LOGO
Global Media Registry

Global Publishers & General Enterprises Limited

Global Publishers & General Enterprises Limited

Global Publishers & General Enterprises Limited ni kampuni binafsi iliyosajiliwa na kushughulikia uchapishaji wa magazeti ya kila siku nchini Tanzania. Kampuni inamiliki magazeti sita ya Amani, Championi, SpotiXtra, Ijumaa, Risasi na Uwazi yenye wito wa “Kampuni ya Magazeti Pendwa”. Magazeti yote yanatumia Kiswahili. Kampuni hii pia inamiliki Online Television inayojulikana kama “Global TV Online”

Maudhui ya magazeti ya Global Publishers & General Enterprises Limited yanahusu siasa, watu mashuhuri, hadithi fupi, burudani, michezo na umbeya, ni mambo yanayosababisha kuwa na aina ya uandishi wa habari za kusisimua za udaku.

Kwa mujibu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) (2018), kampuni ya Global Publishers & General Enterprises Limited inamilikiwa na Joachim Lusana Buyobe kwa 100%. Buyobe pia anamiliki Geita online TV kwa 100%. Hakuna taarifa zaidi kuhusu Buyobe.

Kwa upande wake Eric James Shigongo anaonesha kuhusika kwa karibu na kampuni. Anatajwa kuwa ni Ofisa Mtendaji Mkuu, Mkurugenzi na Msimamizi wa Global Group – wakati mwingine huwa ni mmiliki wa tovuti nyingi. Pia huwa anaitaja kampuni kwenye facebook yake. Nafasi yake haifahamiki kwa sababu wasifu wa kampuni yake haukupatikana katika Wakala ya Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) na kampuni hiyo haikujibu maswali ya mahojiano.

Shigongo amejipatia umaarufu kama mjasiriamali, mwandishi wa vitabu na msemaji. Amezaliwa Mwanza kwenye fukwe za ziwa Victoria, amekuwa na uthubutu wa mambo mengi, ikiwemo vyombo vya habari, hoteli, kilimo, milki na uendelezaji ardhi na majengo.

Kwa mujibu wa utafiti wa GeoPoll (2018), kuhusu kiwango cha wasomaji, Global Publishers & General Enterprises Limited inachapisha magazeti pendwa Tanzania kama vile Champion (XX.XXX%) (ni la 5 kwa wasomaji) pamoja na Risasi na Ijumaa, yenye XX.XXX% kila moja (nafasi ya 13 na 14) kati ya magazeti 28 ikiwemo magazeti makuu yanayochapishwa nchini.

Taarifa muhimu

Aina ya Biashara

Binafsi

Mfumo kisheria

Kampuni ya dhima yenye kikomo

Nyanja za Kibiashara

Global Publishers & General Enterprises Limited imesajiliwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Wakala ya Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) kutoa huduma za magazeti na huduma mtandaoni.

Umiliki

Joachim Lusana Buyobe

Raia wa Tanzania hajionyeshi. Pia anamiliki Geita online TV kwa 100%.

100%
Vyombo vya habari
Other Media Outlets

Magazeti mengine

Amani

Digitali nyingine

globalpublishers.co.tz

Halisia

Chombo cha habari cha kibiashara

Mchapishaji Magazeti

Global Publishers & General Enterprises Limited

Huduma za Maudhui Mtandaoni

Global Publishers and General Enterprises Limited

Maelezo yote

Mwaka wa kuanzishwa

1998

Mwanzilishi

Abdallah Mrisho Salawi hakuna taarifa zaidi kuhusu mwasisi mwenza.
Eric Shigongo - ni mjasiriamali, mwandishi wa vitabu na msemaji. Alizaliwa Mwanza, kwenye fukwe za ziwa Victoria, ana kampuni mbalimbali zikiwemo vyombo vya habari, hoteli, kilimo, uendelezaji milki na nyumba. Ni mwandishi maarufu anayeandika hadithi mfululizo kwenye magazeti na riwaya.

Waajiriwa

Taarifa zisizopatikana

Mawasiliano

Global Publishers & General Enterprises Limited;

P. O. Box 7534, Dar-Es-Salaam;

www.globalpublishers.co.tz

Namba ya kutambulika

BRELA Incorporation N°38971

Taarifa za kifedha

Taarifa ya Kifedha

Taarifa zisizopatikana

Faida za uendeshaji

Taarifa zisizopatikana

Utangazaji(jumla ya mapato kwa asilimia)

Taarifa zisizopatikana

Utawala

Bodi ya utendaji + Bodi Maslahi ya utendaji

Taarifa zisizopatikana

Bodi isiyo ya utendaji + Bodi maslahi isiyo ya utendaji

Taarifa zisizopatikana

Bodi ya usimamizi + Bodi Maslahi ya usimamizi

Taarifa zisizopatikana

Watu muhimu wenye ushawishi + watu maslahi wengine muhimu

Taarifa zisizopatikana

  • Project by
    Media Council of Tanzania
  •  
    Global Media Registry
  • Funded by
    BMZ