This is an automatically generated PDF version of the online resource tanzania.mom-gmr.org/en/ retrieved on 2024/03/29 at 00:14
Global Media Registry (GMR) & Media Council of Tanzania - all rights reserved, published under Creative Commons Attribution-NoDerivatives 4.0 International License.
Media Council of Tanzania LOGO
Global Media Registry

Mwananchi Communications Limited

Mwananchi Communications Limited

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) Tanzania, ambaye pia ni Msajili wa Magazeti nchini, Mwananchi Commmunications Company inamilikiwa na Nation Media Group of Kenya (49%) na Bhalo Jehangir Kermali Bhaloo (51%). Mpaka hivi karibuni, kutokana na matokeo ya dodoso lililojazwa na kampuni yenyewe, Nation Media Group iliwahi kumiliki 99% ya hisa na Linus Githai 1%. Umiliki wa wageni umezidi ukomo cha kisheria cha 49% kilichosababisha mabadiliko ya hivi karibuni katika umiliki.

Mkurugenzi Mtendaji wa MCL ni Francis Majige Nanai na Mkurugenzi Mkuu ni Bakari Machumu.

Kampuni hii inachapisha MWANANCHI, gazeti la Kiswahili la kila siku linaloongoza nchini Tanzania na toleo la Jumapili la MWANANCHI JUMAPILI, na MWANASPOTI, linalotoka mara mbili kwa wiki la michezo na burudani lililoanzishwa 12 Februari 2001. Magazeti ya Kiingereza ni THE CITIZEN na toleo lake la Jumapili la THE SUNDAY CITIZEN. Kampuni pia inachapisha vijarida/magazine nyingi kwa kiingereza na Kiswahili. Machapisho ya kampuni yalikuwa yakichapwa kwa mkataba mpaka 2005, wakati iliponunua mtambo wa uchapishaji uliotumika kutoka Australia.

Historia ya Mwananchi Communications Limited inaweza kufuatiliwa kuanzia mwaka 1999 wakati Balozi Ferdnand Ruhinda alipoanzisha kampuni ya mawasiliano, Media Communication Limited na Aprili 2001 alipoanzisha kampuni mpya aliyoiita Advertising Agency & Public Relations. Hata hivyo, mwaka huo huo (2001) jukumu la uchapishaji lilihamishwa kutoka Media Comminication Limited kwenda kwenye kampuni mpya ya uchapishaji iliyoanzishwa, Mwananchi Communications Limited iliyoanzishwa na balozi Ruhinda kwa ubia na Rostam Aziz. The National Media Group of Kenya ilinunua hisa nyingi. Desemba mwaka 2002 na MCL ikawa kampuni tanzu nchini Tanzania.

Makao yake makuu yapo Kiwanja Na. 34/35 Tabata Relini, Mandela Road, Dar es Salaam, Tanzania.

Taarifa muhimu

Kampuni Mama

Nation Media Group Limited

Aina ya Biashara

Binafsi

Mfumo kisheria

Kampuni ya dhima yenye kikomo

Nyanja za Kibiashara

Mwananchi Communications Limited and Mwanaspoti Nwspaper imesajiliwa TCRA kama mtoa huduma ya maudhui mtandaoni, Malezo na BRELA

Umiliki

Kampuni

Nation Media Group Limited

Kwa mujibu wa BRELA, Kampuni ya Kenya ya National Media Group (NMG) inamiliki 60% ya hisa. Taarifa hii inawezekana imepitwa na wakati kwa sababu umiliki wa kigeni umepunguzwa kwa mujibu wa wawakilishi wa kampuni. NMG inaendeshwa na Aga Khan Foundation na His Highness Aga Khan.

49%
Nation Media Group Limited

Jeangir Kermalzi Bhalov

Raia wa Tanzania. Ana hisa nyingi kwa mujibu wa mwaka 2018.

51%
Vyombo vya habari
Other Media Outlets

Magazeti mengine

Mwananchi

Digitali nyingine

mwananchi.co.tz

Halisia

Chombo cha habari cha kibiashara

Mchapishaji Magazeti

Mwananchi Communications Limited

Huduma za Maudhui Mtandaoni

Mwananchi Communications Limited

Biashara

Ni biashara ya vyombo vya habari tu

Maelezo yote

Mwaka wa kuanzishwa

Registration 2000, Launch 2001

Mwanzilishi

Aziz Rostam - ni mwanasiasa, mfanyabiashara na miongoni mwa Watanzania tajiri sana. alijiuzulu nyadhifa zote za CCM mwaka 2011.
Ruhinda Ferdinand – Alikuwa Balozi wa Jamhuri ya watu wa China. Ni mwanachama wa chama tawala

Waajiriwa

326

Mawasiliano

Mwananchi Communications Limited (MCL);

P.O Box 19754, Dar es Salaam;

Tel.: +255754780647;

Fax: +255222224875;

www.mwananchi.co.tz;

Namba ya kutambulika

TAX ID 100-895-803
BRELA Incorporation N°41222

Taarifa za kifedha

Taarifa ya Kifedha

Taarifa zisizopatikana

Faida za uendeshaji

Taarifa zisizopatikana

Utangazaji(jumla ya mapato kwa asilimia)

Taarifa zisizopatikana

Utawala

Bodi ya utendaji + Bodi Maslahi ya utendaji

Francis Nanai

Bodi isiyo ya utendaji + Bodi maslahi isiyo ya utendaji

Leonard Mussusa

Bodi ya usimamizi + Bodi Maslahi ya usimamizi

Taarifa zisizopatikana

Watu muhimu wenye ushawishi + watu maslahi wengine muhimu

Taarifa zisizopatikana

Maelezo ya ziada

Uwazi hafifu

Upatikanaji wa taarifa za wamiliki kutoka kwenye kampuni/chaneli

3 ♥

Taarifa ya ziada

Wasifu wa Kampuni BRELA umepitwa na wakati (mgongano kuhusu umiliki wa mgeni). Kurudishwa kwa dodoso na hati ya leseni ya Maelezo

  • Project by
    Media Council of Tanzania
  •  
    Global Media Registry
  • Funded by
    BMZ