This is an automatically generated PDF version of the online resource tanzania.mom-gmr.org/en/ retrieved on 2024/03/28 at 10:39
Global Media Registry (GMR) & Media Council of Tanzania - all rights reserved, published under Creative Commons Attribution-NoDerivatives 4.0 International License.
Media Council of Tanzania LOGO
Global Media Registry

E FM

E-FM ni kituo cha redio kinachofanyakazi chini ya kampuni mama ya E-FM Company Limited. Ilianza shughuli zake mwaka 2014.

E-FM ni kituo cha redio kinachotangaza saa 24 free to air na kituo cha redio cha biashara chenye makao yake makuu Dar es Salaam, Tanzania. Vipindi vya E-FM vinatangaza masuala mbalimbali kuanzia habari, michezo, matukio, vipindi maalumu (vya nchini na vya kimataifa), mitindo ya maisha, burudani na vinginevyo.

Kama ilivyoelezwa na ripoti ya Tanzania Media Measurement na GeoPoll, kwa takwimu za robo mwaka ya pili ya mwaka 2018, Redio E-FM ni ya tatu kwa idadi ya wasikilizaji XX.XXX%  miongoni mwa vituo 20 vya redio nchini Tanzania.

Tehehe 2 Aprili, 2014 E-FM ilianza kutangaza kwa majaribio na kuanza utangazaji rasmi mwaka huo huo, na kuwa redio ya burudani maarufu miongoni mwa wasikilizaji vijana wa Dar es salaam na mikoa mingine 8 nchini.

E-FM Company Limited pia inamiliki kituo cha TV kijulikanacho kama TVE. Kwa mujibu wa taarifa kutoka Wakala ya Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na vyanzo vingine, zilionesha kuwa kampuni hii inamilikiwa na ndugu watatu, ambapo Francis Antony Ciza anamiliki 40% ya hisa, Jean Claude Ciza 40% ya hisa na Justine Antoine Ciza anamiliki 20% ya hisa. Wao ni Wanahisa na Wakurugenzi.

Licha ya kuwa miongoni mwa wanahisa na mtendaji mkuu wa E-FM Company Limited, Francis Antony Ciza anamiliki zaidi ya Nigh Club moja zilizopo katika mikoa mbalimbali nchini. Aliwahi kuwa DJ katika redio ya Magic FM.

Taarifa muhimu

Isa za hadhira

Aina ya umiliki

binafsi

Maeneo yanayofikiwa

Taifa

Aina ya maudhui

Maudhui huru

Taarifa zinazopatikana kiurahisi

Upatikanaji wa taarifa za umiliki kutoka kwa vyanzo vingine, kwa mfano vile vinavyotambulikana kisheria

2 ♥

Kampuni ya vyombo vya Habari

E-FM Company Limited

Umiliki

Muundo wa umiliki

TV E inaendeshwa na E-FM Company Limited, inayomilikiwa na familia ya Ciza..

Haki ya kuchagua

Taarifa zisizopatikana

Mmiliki Binafsi

Kampuni ya vyombo vya Habari
Halisia

Maelezo yote

Mwaka wa kuanzishwa

Start: April 2014 on a trial basis

Mwanzilishi

Justina Antoine Ciza. Francis Antony Ciza. Jean Claude Ciza.

Mtendaji Mkuu

Francis Antony Ciza - anamiliki zaidi ya Night Club Moja kwenye mikoa ya mbalimbali nchini, pia alikuwa DJ wa Magic FM radio.

Mhariri Mkuu

Scholastica Mazula - mwandishi wa habari - Aliwahi kufanyakazi Times Redio

Mawasiliano

E-FM Company Limited

P.O. Box 71476, Dar-Es-Salaam

Tel.: +255222780320

E-Mail: info@efm.co.tz

Taarifa za kifedha

Taarifa ya Kifedha

Taarifa zisizopatikana

Faida za uendeshaji

Taarifa zisizopatikana

Utangazaji(jumla ya mapato kwa asilimia)

Taarifa zisizopatikana

Isa katika soko

Taarifa zisizopatikana

Maelezo ya ziada

  • Project by
    Media Council of Tanzania
  •  
    Global Media Registry
  • Funded by
    BMZ