This is an automatically generated PDF version of the online resource tanzania.mom-gmr.org/en/ retrieved on 2024/04/23 at 11:05
Global Media Registry (GMR) & Media Council of Tanzania - all rights reserved, published under Creative Commons Attribution-NoDerivatives 4.0 International License.
Media Council of Tanzania LOGO
Global Media Registry

Jamii Forum

Jamii Forum ni mtandao wa kijamii wa Tanzania ulianzishwa kama Jambo Forums katika miaka ya 2006. Unafanya kazi chini ya Jamii Forums Company Limited iliyosajiliwa Julai 2008.

Kwa mujibu wa Maxence Melo, Mwasisi-mwenza na mmiliki-mwenza, Jamii Forums imetokana na Jambo Forums iliyokuwa na majukwaa madogo mengi ya mtandaoni kama vile Tanzania Economic Forums, Habari Tanzania, Uchaguzi Tanzania, Jambo Network, Jambo Redio na Jambo Video.

Kusudio kuu la kuanzisha Jamii Forums, kwa mujibu wa Melo, ni kuunda jukwaa ambapo jamii ya kitanzania inaweza kushiriki kwenye mjadala huru kuhusu masuala mbalimbali yanayojitokeza kama vile ya kijamii kisiasa, kiuchumi na ripoti za habari zinazotokea hivi punde.

Kulingana na utafiti wa GeoPoll kuhusu matumizi ya mitandao, uliyodhaminiwa MCT, Jamii Forums ni tovuti ya kwanza kwa habari yenyeXX.XXX% ya hadhira. Kwa mujibu wa Alexa Traffic, ni ya tano miongoni mwa mitandao ya kijamii nchini (Oktoba, 2018). Taarifa ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) inasema kwamba, mtandao huo una watumiaji 2.4 milioni,walipiaji wa simu za mkononk 2.8 milioni na takribani watu 600,000 wanaotumia mtandao huu wa kijamii kila siku, mwezi Agosti 2017.

Maudhui ya Jamii Forums yanashughulikia habari za kawaida na hutoa fursa ya majadiliano ya masuala mbalimbali ya kijamii, kiuchumi, kisiasa, michezo na burudani. Licha ya kwenye blog hii, habari zipo kwenye Google Play, Instagram, Facebook, Twitter @Jamii Forums, pamoja na Youtube.

Mwezi Juni 2018, Jamii Forums ilifungiwa kutokana na wamiliki wake kuchelewa kulipa ada ya usajili kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) iliyotakiwa kulipwa kulingana na kanuni mpya ya maudhui ya mtandaoni (Online Internet Regulation). Kwa mujibu wa kanuni hii mpya, wamiliki wa blog/majukwaa ya mtandaoni wana wajibu wa kulipa hadi Tsh 2.1 milioni, pamoja na Tsh 1 milioni kwa ada ya Leseni ya awali kabla ya kuanza kuendesha forums zao. Wanatakiwa pia wataje taarifa za wanahisa wao, uraia wao na mtaji wa hisa.

Kanuni hiyo pia inawataka wamiliki wa blog na waendeshaji wa Forums kujisajili TCRA, kuhakikisha kuwa maoni yanayotolewa na wasomaji wa blog, watumiaji wa Forums ni ya wastani kabla ya kuchapishwa. Aidha wanatakiwa pia kubainisha chanzo cha maudhui.

Melo alieleza kuwa vyombo vya habari kuhusu kufungiwa huko:”Tumelengwa kwa sababu Forum yetu ni mtoa huduma na si mtoa maudhui, kwa hiyo tuliamua kufunga kwa sababu hatuna nafasi yoyote (kwenye kanuni za maudhui ya mtandao)”.

Mwezi Julai 2018, TCRA ilitoa Online Content Services Licence kwa Jamii Forums kwa hiyo iliendelea kutoa huduma baada ya kutimiza matakwa ya kanuni hiyo.

Kwa mujibu wa maelezo ya kampuni zenyewe, kampuni inayoendesha shughuli zake iliasisiwa na kumilikiwa na Maxence Melo Mubyazi (51%) na Mike Mushi (49%)

Taarifa muhimu

Isa za hadhira

Aina ya umiliki

Binafsi

Maeneo yanayofikiwa

Kimataifa

Aina ya maudhui

Maudhui huru

Taarifa zisizopatikana

Taarifa za wamiliki wa vyombo vya Habari ambazo hazikupatikana, kampuni zakataa kutoa maelezo au hazikujibu au hazina hifadhi ya kumbukumbu zake

1 ♥

Kampuni ya vyombo vya Habari

Jamii Media Co. Limited

Umiliki

Muundo wa umiliki

Jamii Forum ni Mtoa Taarifa Mtandaoni iliyosajiliwa TCRA. Katika TCRA, ni Melo tu ndiye aliyetajwa kama mmiliki wa hisa. Kwenye akaunti zao wenyewe pia Mushi anamiliki hisa zilizobaki.

Haki ya kuchagua

Taarifa zisizopatikana

Mmiliki Binafsi

Kundi / Mmiliki Binafsi

Mike Mushi

Muasisi mbia wa Jamii Forums tangu alipokuwa na umri wa miaka 16 tu. Alianza kusimamia Jamii Forums mara tu alipomaliza shule ya msingi ya Green Acres mwaka 2003. Hivi sasa ni Mkurugenzi na Mkuu wa Ubia wa Biashara na Masoko katika Jamii Media. Amesoma shahada ya Business Administration with Information Technology katika Learn IT kuanzia mwaka 2010 mpaka 2013.

49%
Kampuni ya vyombo vya Habari
Halisia

Maelezo yote

Mwaka wa kuanzishwa

2nd July, 2008

Mwanzilishi

Maxence Melo – ana Shahada ya Kwanza ya Sayansi (BSc) katika Uhandisi Majengo na amefanyakazi katika kampuni ya ujenzi kabla ya kuanzisha kwa ubia Jamii Forums. Pia ni mwanaharakati wa kidijitali anayehamasisha uhuru wa kutoa mawazo, usalama wa kidijital

Mtendaji Mkuu

Maxence Melo - angalia hapo juu

Mhariri Mkuu

Hakuna taarifa kuhusu chumba cha habari

Mawasiliano

P. O. Box 4203

DAR ES SALAAM

maxence@jamiiforums.com

Tel:+255 758525253

Taarifa za kifedha

Taarifa ya Kifedha

Taarifa zisizopatikana

Faida za uendeshaji

Taarifa zisizopatikana

Utangazaji(jumla ya mapato kwa asilimia)

Taarifa zisizopatikana

Isa katika soko

Taarifa zisizopatikana

Maelezo ya ziada

Taarifa ya ziada

Idadi ya hadhira kwa mujibu wa utafiti wa GeoPoll (Aug 30 – Sep 1st, 2018), uliyodhaminiwa na MOM Tanzania. Mitandao ya kijamii, tovuti za kutafuta habari, na tovuti za matangazo hazikuingizwa kwenye uchambuzi wa umiliki.

  • Project by
    Media Council of Tanzania
  •  
    Global Media Registry
  • Funded by
    BMZ