This is an automatically generated PDF version of the online resource tanzania.mom-gmr.org/en/ retrieved on 2024/04/16 at 15:51
Global Media Registry (GMR) & Media Council of Tanzania - all rights reserved, published under Creative Commons Attribution-NoDerivatives 4.0 International License.
Media Council of Tanzania LOGO
Global Media Registry

Millardayo.com

Millardayo.com ni miongoni mwa tovuti ya habari nchini Tanzania inayoendeshwa na kumilikiwa na Millard Afrael Ayo na ndugu yake. Tovuti hiyo imeanzishwa mwaka 2012 na Ayo na kuipa jina lake.

Kuanzishwa kwa Millardayo.com kumechangiwa zaidi na Issa Michuzi, mwendesha blog mkubwa nchini Tanzania, na Ambwene Yesaya ambaye ni mwanamziki maarufu nchini Tanzanian na rafiki mkubwa wa Ayo. Walimshauri aanze blog kuhusu visa na habari alizokuwa akizitangaza Clouds FM radio kwa kuwasaidia wale waliokosa kusikiliza redio.

Millardayo.com ilitajwa kama njia ya pili maarufu kupasha habari kwenye utafiti uliyogharimiwa na MCT (Aug/Sep) wa GeoPoll kuwa na hadhira ya XX.XXX%.  Pia kwa mujibu wa Alexa Traffic, Millardayo.com ilikuwa ya 19 (Oct 2018). Maudhui ya Millardayo.com yanahusu habari za kawaida kama vile za nchini, kanda na kimataifa, habari za burudani, kijamii, kisiasa na habari za maisha ya watu binafsi (umbeya)

Hivi sasa Millard Ayo inasimamia na kuajiri zaidi ya wafanyakazi 13 wanaofanyakazi kama waandishi na wapiga picha. Licha ya blog hii (Millardayo.com), habari zinaweza kupatikana YouTube, Google Play & Apple Store, Facebook Twitter @millardayo na Instagram zenye wasomaji 3.9 milioni.

Mwaka 2012, Millardayo.com ilishinda tunzo mbili kutoka nyota wa Africa na Vodacom kuwa tovuti bora zaidi Tanzania.

Blog hiyo inaendeshwa chini ya Ayo TV TZA Company Limited iliyoanzishwa na kumilikiwa na Millard Afrael Ayo (anamiliki hisa 900) na Ivan Ayo (anamiliki hisa 100).

Taarifa muhimu

Isa za hadhira

Aina ya umiliki

Binafsi

Maeneo yanayofikiwa

Kimataifa

Aina ya maudhui

Maudhui huru

Taarifa zinazopatikana kiurahisi

Upatikanaji wa taarifa za umiliki kutoka kwa vyanzo vingine, kwa mfano vile vinavyotambulikana kisheria

2 ♥

Kampuni ya vyombo vya Habari

AYO TV TZA Company Limited

Umiliki

Muundo wa umiliki

Millardayo ni Mtoa Taarifa Mtandaoni iliyosajiliwa TCRA, imeanzishwa na kumilikiwa kwa ubia na Millard A. Ayo.

Haki ya kuchagua

Taarifa zisizopatikana

Mmiliki Binafsi

Kundi / Mmiliki Binafsi

Ivan Ayo

ndugu yake Millard A. Ayo.

10%
Kampuni ya vyombo vya Habari
Halisia

Maelezo yote

Mwaka wa kuanzishwa

2012

Mwanzilishi

Millard Afrael Ayo - alizaliwa tarehe 16 Januari, 1986 nchini Tanzania. Alianza kufanyakazi kama mtaalamu wa vyombo vya habari na kuanzisha kwa ubia blogi yake iliyojipatia tuzo. Bado anaendelea kufanyakazi na Clouds Media kama mtangazaji.

Mtendaji Mkuu

Millard Afrael Ayo - angalia hapo juu

Mhariri Mkuu

Hakuna taarifa kuhusu chumba cha habari

Mawasiliano

P. O. Box 3842

DAR ES SALAAM

ayotvtzacompany@gmail.com

Tel: +255655141619

Taarifa za kifedha

Taarifa ya Kifedha

Taarifa zisizopatikana

Faida za uendeshaji

Taarifa zisizopatikana

Utangazaji(jumla ya mapato kwa asilimia)

Taarifa zisizopatikana

Isa katika soko

Taarifa zisizopatikana

Maelezo ya ziada

Taarifa ya ziada

AIdadi ya hadhira kwa mujibu wa utafiti wa GeoPoll (Aug 30 – Sep 1st, 2018), uliyodhaminiwa na MOM Tanzania. Mitandao ya kijamii, tovuti za kutafuta habari, na tovuti za matangazo hazikuingizwa kwenye uchambuzi wa umiliki.

  • Project by
    Media Council of Tanzania
  •  
    Global Media Registry
  • Funded by
    BMZ