This is an automatically generated PDF version of the online resource tanzania.mom-gmr.org/en/ retrieved on 2024/04/16 at 13:54
Global Media Registry (GMR) & Media Council of Tanzania - all rights reserved, published under Creative Commons Attribution-NoDerivatives 4.0 International License.
Media Council of Tanzania LOGO
Global Media Registry

Radio Maria

Radio Maria Tanzania ni kituo cha redio, kinachotangaza kutoka Dar es salaam kama sehemu ya mtandao wa vituo vya Redio vya Milan, Italy. Muundo wa vipindi vya Redio Maria Tanzania una makundi manne kama vile maarifa ya kiroho ya Watakatifu, habari na taarifa, uhamasishaji na ustawi wa mwanadamu, na mwisho ni jamii na burudani. Mara nyingi hupiga muziki wa Kikatoloki, Kikristo na Injili.

Kwa mujibu wa Ng’atigwa (2013),Radio Maria Tanzania (inayojulikana kwa RMT) na wito wa “Sauti ya Kikristo Nyumbani Kwako” nin kituo cha Redio cha FM kilichoanziswa mwaka 1996 manispaa ya Songea, kusini ya Tanzania. Kuanzishwa kwa RMT ni juhudi zilizofanywa na Archbishop Norbert Mtega, Jimbo la Askofu Mkuu wa Katoliki la Songea wakati wa mkutano wake na Rais wa Association of the World Family of Radio Maria, Italy, Uganda mwaka 1996. Kwa mujibu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), RTM inamilikiwa na World Family Radio Maria Africa kwa 51% na Fondazione Formore kwa 48% zilizobaki.

RMT inamilikiwa na kusimamiwa na The Association of Radio Maria Tanzania Company Limited. Wanachama wa The Association of Radio Maria Tanzania ni pamoja na “watu waliooa, kuolewa na wasioolewa na kuoa, maburuda na watawa, na makasisi na mapadre, hata hivyo, redio hii haimilikiwi na jimbo la askofu la katoliki lolote mahususi nchini Tanzania au mkutano na Maaskofu Tanzania.

Kutokana na matatizo ya vifaa, mahitaji ya uendeshaji huko Songea, RMT imehamishia studio yake kuu eneo la Mikocheni, jijini Dar es salaam mwaka 2003. Kituo kilisajiliwa na TCRA katika kundi la leseni isiyo ya kibiashara, kuendesha kama kituo cha redio cha dini na kuweka kipaumbele cha maudhui na malengo ya dini. Kama sharti la kundi hili la leseni, matangazo ya biashara ni marufuku.

Kwa mujibu wa hadhira/wasikilizaji katika utafiti wa GeoPoll (2018), Radio Maria ni ya 10 yenye XX.XXX%  ya wasikilizaji miongoni mwa vituo 20 nchini Tanzania, na katika kanda ya kati kuna XX.XXX% ikilinganishwa na vituo vya redio vya dini vingine nchini.

HAdi Julai, 2011, RMT imefikia majimbo ya Askofu 13 kati ya Majimbo 33 ya Askofu ya Katoliki nchini Tanzania. Hata hivyo, kupitia matangazo yake kwa satelaiti yaliyoongezwa nguvu na transmita nane zilizopo kwenye maeneo tofauti ya Tanzania, matangazo ya kituo cha redio yanasikika takribani Tanzania nzima. RMT pia hupatikana kwenye mtandao kwa www.radiomaria.co.tz na kuweza kupatikana kwa kutumia ujumbe kwenye akaunti ya facebook.

Taarifa muhimu

Isa za hadhira

Aina ya umiliki

Binafsi isiyo ya biashara

Maeneo yanayofikiwa

Mkoani

Aina ya maudhui

Maudhui huru

Taarifa zinazopatikana kiurahisi

Upatikanaji wa taarifa za umiliki kutoka kwa vyanzo vingine, kwa mfano vile vinavyotambulikana kisheria

2 ♥

Kampuni ya vyombo vya Habari

World Family of Radio Maria Africa

Umiliki

Muundo wa umiliki

Radio Maria inaendeshwa na World Family of Radio Maria Africa ambayo ni mali ya World Family of Radio Maria.

Haki ya kuchagua

Taarifa zisizopatikana

Kundi / Mmiliki Binafsi

Fondazione Formare

48%
Kampuni ya vyombo vya Habari
Halisia

Maelezo yote

Mwaka wa kuanzishwa

Date of registration: May 3rd 1996 Start: April 26th 1996

Mwanzilishi

Askofu Norbert Mtega / Jimbo la Askofu Mkuu wa Katoliki la Songea .

Mtendaji Mkuu

Taarifa zisizopatikana

Mhariri Mkuu

Taarifa zisizopatikana

Mawasiliano

Radio Maria

P. O. Box 34573, DAR ES SALAAM.

info.tan@radiomaria.org

Tel: +255 22 277 3837

Taarifa za kifedha

Taarifa ya Kifedha

Taarifa zisizopatikana

Faida za uendeshaji

Taarifa zisizopatikana

Utangazaji(jumla ya mapato kwa asilimia)

Taarifa zisizopatikana

Isa katika soko

Taarifa zisizopatikana

  • Project by
    Media Council of Tanzania
  •  
    Global Media Registry
  • Funded by
    BMZ