Sahara Media Group Limited
Sahara Media Group (SMG) iliyokuwa ikiitwa Sahara Communication and Publishing Company Limited ni miongoni mwa kampuni za vyombo vya habari zinazoongoza nchini Tanzania. SMG ilianzishwa mwaka 1992 baada ya biashara huru wakati vyombo vya habari vingi vya binafsi vilipoanza nchini Tanzania. Tangu ilipoanzishwa, Sahara Media Group, yenye makao makuu yake Mwanza, mji mkuu wa pili Tanzania kwenye Ziwa Victoria, imekuwa hadi kuwa miongoni mwa kampuni za vyombo vya habari inayoongoza nchini Tanzania na Africa Mashariki na Kati. Kampuni hiyo inatoa huduma za vyombo vya habari zifuatazo: Matangazo kwa njia ya Televisheni na redio; Matangazo mubashara; Huduma za kukodisha Gari la Matangazo ya Nje; Huduma za matangazo ya TV za kidijiti na matangazo kwa njia ya Satellite.
Kampuni hii ya vyombo vya habari inaendesha Star TV, Radio Free Africa na Kiss FM. Pia iliwahi kuchapisha magazeti ya Kiswahili ya kila wiki (Msanii Africa na Sauti ya Afrika) Weekly mail na Usanii. Hata hivyo yalifungwa kutokana na mauzo madogo.
Mpaka wakati tunaandika habari hizi, data za SMG hazikuweza kupatikana katika Wakala ya Usajili wa Biashara na Utoaji wa Leseni (BRELA). Dr. Anthony Diallo ni miongoni mwa waasisi wa SMG, ni mwanachama wa Chama tawala na kwa sasa ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza. Kwa mujibu wa wasifu wake ulivyounganishwa kwenye mtandao, yeye bado ni Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo tangu mwaka 2010.
Diallo, aliyezaliwa 25 Desemba mwaka 1959, ametoa huduma katika nyadhifa mbalimbali kwenye chama na Serikali. Alikuwa mbunge kuanzia mwaka 1995 hadi 2010. Mpaka mwaka 2008 alikuwa Waziri wa Mifugo pamoja na Maliasili na Utalii, kabla ya kuacha uwaziri ili aweze kuendesha biashara zake zaidi, zinazojumuisha magazeti, na kuimarisha utendaji wa vyombo vya habari.
Kwa mujibu wa dodoso lilitayarishwa na R &D manager wa SMG, hakuna utafiti uliofanywa kutathmini mapato ya matangazo kwa kila kituo cha FTA. Serikali inaipa kampuni hiyo habari na taarifa, hata hivyo haisaidii sana katika matangazo ya taifa.
Aina ya Biashara
Binafsi
Mfumo kisheria
Kampuni ya dhima yenye kikomo
Nyanja za Kibiashara
Utangazaji
Mmiliki Binafsi
Hakuna wasifu wa kampuni BRELA. Wamiliki wa hisa inawezekana wasiwe sahihi. Dialloni mwanasiasa wa CCM na inaelekea kuwan ni muasisi na mmiliki na Ofisa Mtendaji Mkuu
Magazeti mengine
Msanii Afrika (closed)
Sauti ya Africa (closed)
Televisheni zingine
Star TV
Radio nyingine
Radio Free Africa
Kiss FM
Digitali nyingine
registered as a Online Content Service at TCRA.
Chombo cha habari cha kibiashara
Broadcasting
Sahara Media Group Limited
Biashara
none
none
Maelezo yote
Mwaka wa kuanzishwa
1992
Mwanzilishi
Dr. Anthony M. Diallo - is a politician and Mwanza Regional Party Chairman of the ruling Chama cha Mapinduzi (CCM). He was a Member of Parliament (1995 to October 2010) when he lost to the opposition candidate. He served in different capacities in the cabinet from 2000 to 2008.
Waajiriwa
204
Mawasiliano
Plot No. 5-7, Ilemela Industrial Area
Airport Road,
P.O Box 1732,
Mwanza
Namba ya kutambulika
BRELA incorporation n°: 179974
Taarifa za kifedha
Taarifa ya Kifedha
Taarifa zisizopatikana
Faida za uendeshaji
Taarifa zisizopatikana
Utangazaji(jumla ya mapato kwa asilimia)
Taarifa zisizopatikana
Utawala
Bodi ya utendaji + Bodi Maslahi ya utendaji
Taarifa zisizopatikana
Bodi isiyo ya utendaji + Bodi maslahi isiyo ya utendaji
Taarifa zisizopatikana
Bodi ya usimamizi + Bodi Maslahi ya usimamizi
Taarifa zisizopatikana
Maelezo ya ziada
Taarifa ya ziada
No company profile available at BRELA. Registered at TCRA, no shareholders. mentioned. No return of questionnaire.
Ayub Rioba (2008). Media in Tanzania’s Transition to multiparty Democracy: An assessment of Policy and Ethical issues, Lacentiate’s Thesis. University of Tampere.