This is an automatically generated PDF version of the online resource tanzania.mom-gmr.org/en/ retrieved on 2024/03/29 at 00:50
Global Media Registry (GMR) & Media Council of Tanzania - all rights reserved, published under Creative Commons Attribution-NoDerivatives 4.0 International License.
Media Council of Tanzania LOGO
Global Media Registry

Azam Two

Azam TV ni mtoa huduma binafsi kwa njia ya dijiti kupitia Satelaiti iliyopo Dar es salaam na kumilikiwa na Azam Media Limited, kampuni tanzu ya Bakhresa Group Companies. Azam TV imeanzishwa mwaka 2013, na kuwa miongoni vya vituo vya TV vyenye hadhira kubwa. Ni ya tatu nchini kwa kuwa na watazamaji wengi, XX.XXX% kwa mujibu wa utafiti war obo ya pili ya mwaka 2018, utafiti wa GeoPoll.

Ina vipindi vingi vikiwemo filamu, vipindi vya uhalisia, filamu za burudani ndefu, vipindi vya elimu, michezo na habari na matukio. Kituo hiki kinajivunia cheneli tatu zinazokidhi mahitaji ya aina zote za hadhira na hivyo kuwa miongoni mwa TV zinazopendwa kuangaliwa sana na makundi yote ya jamii.

Chaneli hizo ni: Azam One, inayoshughulikia vipindi vya makala kama vile Semina za Kiafrika, mechi za mpira na burudani kwa watoto; Azam Two, ni chaneli ya burudani ya kimataifa ambapo watazamaji watapata tamthilia, makala, mziki, sinema za mapenzi na Sinema Zetu inayotoa sinema mbalimbali a Bongo.

Azam Media Limited inasimamiwa na Yusuf Said Salim Bakhresa, miongoni mwa watoto wane wa mwasisi wa Bakhresa Group. Kwa mujibu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania–TCRA, Yusuf Said pia ni mwanahisa wa Azam Media Limited kama walivyo ndugu zake Abubakar Said Salim Bakhresa, Omar Said Salim Bakhresa na Mohamed Said Salim Bakhresa. Kila mmoja anamiliki 5% ya hisa, wakati Said Salim Bakhresa & Co Ltd – ambayo pia ni kampuni tanzu ya Bakhresa Group of Companies anamiliki 80% ya hisa zilizobaki.

Azam Media is imesajiliwa, Wakala ya Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) (N0.95870) na jalada la kampuni lilipatikana. Limeorodhesha wanahisa waliotajwa hapo juu, pia imetaja rehani tarehe 12 Juni, 2013 kwa Standard Chartered Bank Tanzania Limited kupata USD 8,000,000. Mapato ya kila mwaka yameripotiwa hadi 2017.

Taarifa muhimu

Isa za hadhira

Aina ya umiliki

Binafsi

Maeneo yanayofikiwa

Taifa

Aina ya maudhui

Free to Air

Taarifa zinazopatikana kiurahisi

Upatikanaji wa taarifa za umiliki kutoka kwa vyanzo vingine, kwa mfano vile vinavyotambulikana kisheria

2 ♥

Kampuni ya vyombo vya Habari

Azam Media Limited

Umiliki

Muundo wa umiliki

Azam Two inaendeshwa na Azam Media Limited inayomilikiwa na kampuni ya familia ya Bakhresa Group.

Haki ya kuchagua

Taarifa zisizopatikana

Mmiliki Binafsi

Kampuni ya vyombo vya Habari
Halisia

Maelezo yote

Mwaka wa kuanzishwa

2013

Mwanzilishi

Said Salim Awadh Bakhresa - ni mfanyabiashara mwenye mafanikio na uzoefu wa zaidi ya miaka 30 ya kusimamia kampuni yenye biashara mbalimbali. Ni muasisi na Mwenyekiti wa Bakhresa Group of Companies.

Mtendaji Mkuu

Yusuf Said Salim Bakhresa - ni Mkurugenzi Mtendaji wa Azam Media Limited na pia ni Mkurugenzi wa the Group Companies. Anashiriki kwa ukamilifu katika shughuli za kila siku za Bakhresa food products Ltd. Yeye ni mtoto wa Said Salim.

Mhariri Mkuu

Tido Mhando - ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji. Aliwahi kufanyakazi na BBC Swahili Service mapema miaka ya 2000 kabya ya kujiunga na TBC kama Mtendaji Mkuu.. Kabla ya kujiunga na BBC, alifanyakazi Voice of Kenya (VoK) iliyopo Nairobi na Radio Tanzania Dar e

Mawasiliano

Azam Media Limited

P.O. Box: 2517, Dar-Es-Salaam

Tel.: +255687030580

E-Mail: hassan.mhelela@azam-media.com

www.azamtv.co.tz

Taarifa za kifedha

Taarifa ya Kifedha

Taarifa zisizopatikana

Faida za uendeshaji

Taarifa zisizopatikana

Utangazaji(jumla ya mapato kwa asilimia)

Taarifa zisizopatikana

Isa katika soko

Taarifa zisizopatikana

Maelezo ya ziada

Taarifa ya ziada

Kiwango cha hadhira kwa mujibu wa ripoti ya viwango vya GeoPoll ya Redio & TV (Aprili – Juni 2018).

  • Project by
    Media Council of Tanzania
  •  
    Global Media Registry
  • Funded by
    BMZ