East Africa Radio
East Africa Radio (EA FM) ni radio ya burudani kwa saa 24 (Free to air – FM Radio Station). Inatangaza kutoka Dar es salaam, matangazo yake yanapokewa kupitia satelaiti hadi Nairobi na Kampala, inakotangaza kutoka nchini huko. Vipindi vya EA FM vinashughulikia masuala mbalimbali kuanzia habari, matukio, ( ya nchini na kimataifa), mitindo ya maisha, burudani na mengineyo.
Kwa mujibu wa ripoti ya Tanzania Media Measurement iliyofanywa na GeoPoll, kwa kutumia takwimu za wasikilizaji za robo mwaka ya 2, 2018, EA FM ina wasikilizaji XX.XXX%. Ina maana kwamba ni ya sita miongoni mwa vituo vyote vya redio.
Katika Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) HAKUNA TAARIFA ZOZOTE KUHUSU EA FM. Anuwani yake ya biashara inaelekeza East Africa Television Limited na EA FM ilianza shughuli zake pamoja na EATV - kwa hiyo uhusiano wao ni sahihi. Ni kampuni shiriki ya IPP Limited.
IPP Group Limited ni kampuni ya utengenezaji, utiaji vinywaji kwenye chupa na kundi la vyombo vya habari inayojumuisha vituo vya Televisheni, redio na magazeti. Wasifu wa kampuni uliyoombwa kwa Wakala wa Usajili wa Biashara na Utoaji wa Leseni (BRELA) unaonyesha kuwa Dkt Reginald Abraham Mengi na Agaptus Leon Nguma ni wanahisa wa IPP Group Limited.
Mengi alizaliwa Tanzania mwaka 1944, yeye ni mfadhili wa Kitanzania, mwana viwanda, mmiliki wa vyombo vya habari na mwasisi na mwenyekiti Mtendaji wa IPP Group. Mengi pia ni Makamu wa Rais wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi (NBAA) Tanzania. Katika taarifa ya FORBES, amekuwa ni miongoni mwa matajiri wa Afrika mwenye zaidi ya $400 Millioni kwa takwimu za 2015.
Isa za hadhira
Aina ya umiliki
binafsi
Maeneo yanayofikiwa
Taifa
Aina ya maudhui
Maudhui huru
Kampuni ya vyombo vya Habari
IPP Media Limited
Muundo wa umiliki
East Africa Radio inaendeshwa na IPP Media Ltd., inayomilikiwa na Dr. Reginald Mengi. Wamiliki wa hisa na hisa zao havikupatikana TCRA.
Haki ya kuchagua
Taarifa zisizopatikana
Mmiliki Binafsi
Kundi / Mmiliki Binafsi
Agapitus Leons Nguma
likuwa katibu wa kampuni na mwanahisa. Amefariki dunia 1 Mei 2018. Alikuwa pia Mkurugenzi wa the Guardian Ltd.na Bonite Bottlers Ltd. Kitaaluma ni Mwanasheria.
Maelezo yote
Mwanzilishi
Dr. Reginald Mengi - ni mwanaviwanda wa Tanzania, mmiliki wa vyombo vya habari na muasisi, pia ni Mwenyekiti mtendaji wa IPP Group. Pia ni Makamu wa Rais wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi Tanzania. Katika taarifa za FORBES, Mengi ni miongoni mwa mt
Mtendaji Mkuu
Regina Mengi - Mkurugenzi Mtendaji. Ni binti wa Dkt. Mengi.
Mhariri Mkuu
Nasser Kingu - Mkuu wa Vipindi
Mawasiliano
Taarifa za kifedha
Taarifa ya Kifedha
Taarifa zisizopatikana
Faida za uendeshaji
Taarifa zisizopatikana
Utangazaji(jumla ya mapato kwa asilimia)
Taarifa zisizopatikana
Isa katika soko
Taarifa zisizopatikana
Maelezo ya ziada
Taarifa ya ziada
Kiwango cha hadhira kwa mujibu wa ripoti ya viwango vya GeoPoll ya Redio & TV (Aprili – Juni 2018).
Muhtasari wa vyombo vya habari
Reginald Abraham Mengi (2018), I Can, I must, I will. ISBN-10: 9781717871749.