ITV
Independent Television Limited ni kampuni tanzu/shiriki IPP Limited. ITV ilianza shughuli zake mwaka 1994 ikiwa na kituo kimoja cha televisheni na kimoja cha redio kinachojulikana kuwa ITV (Independent Television Limited) na Radio One, mtawalia.
ITV ni Free to Air Chanel nchini Tanzania bara, pia ni kituo cha TV cha biashara kinachotangaza kupitia masafa bora (VHF). Ripoti ya GeoPoll’s Tanzania Media Measurement yenye takwimu za hadhiri za robo mwaka ya pili ya 2018 zinazopimia utazamaji wa Vituo vya TV vinavyotazamwa sana na vituo vya radio vinavyosikilizwa sana nchini, imeiweka kituo cha ITV kuwa na hisa ya hadhira ya XX.XXX% na kuwa namba moja miongoni mwa vituo vya TV vyote nchini Tanzania.
Kwa mujibu wa kampuni yenyewe, taarifa ya bahari ya saa 2:00 usiku (20:00 HRS) ndiyo inayoongoza kwa kuwa na watazamaji takribani 70% siku yoyote ile. Taarifa ya habari hutangaza habari za nchini, za kimataifa, za biashara na za michezo pia ITV inatangaza habari za nchini saa 12:00 asubuhi (06:00 HES) kuanzia Jumatatu hadi Jumapili na saa 5:00 usiku (23:00 HRS) Jumatatu mpaka Ijumaa. Licha ya hivyo, kituo hicho kinatangaza habari za saa kwa dakika tano kuanzia saa 2:55 asubuhi (08:55 HRS) mpaka saa 9:55 asubuhi na matangazo yake kusikika barani Afrika sehemu za mashariki ya kati na Ulaya. Zaidi ya 60% ya vipindi vyake ni vya nchini vinavyolenga familia yote na kujuisha umri wote na hali ya uchumi jamii.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Reginald Abraham Mengi na IPP Group Limited ni wamiliki wa Independent Television Limited (ITV). Mengi pia ni mtendaji Mkuu.
IPP Group Limited ni kampuni ya utengenezaji utiaji vinywaji kwenye chupa na kundi la vyombo vya habari inayojumuisha vituo vya televisheni na vya redio na magazeti. Wasifu wa kampuni uliyoombwa kwa Wakala wa Usajili wa Biashara na Utoaji wa Leseni (BRELA) unaonyesha kuwa Dkt Reginald Abraham Mengi na Agaptus Leon Nguma ni wanahisa wa IPP Group Limited.
Mengi alizaliwa Tanzania mwaka 1944, yeye ni mfadhili wa Kitanzania, mwana viwanda, mmiliki wa vyombo vya habari na mwasisi na mwenyekiti Mtendaji wa IPP Group. Mengi pia ni Makamu wa Rais wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi (NBAA) Tanzania . Katika taarifa ya FORBES, amekuwa ni miongoni mwa matajiri wa Afrika mwenye zaidi ya $400 Millioni kwa takwimu za 2015.
Isa za hadhira
Aina ya umiliki
Binafsi
Maeneo yanayofikiwa
Taifa
Aina ya maudhui
Free to Air
Kampuni ya vyombo vya Habari
IPP Media Limited
Muundo wa umiliki
IPP Media ni mali ya IPP Group, kampuni binafsi inayomilikiwa na kikundi cha kampuni zilizoanzishwa na Dr. Reginald Abraham Mengi miaka ya 1960. Mmiliki hisa hawakuoneshwa TCRA, Julai 2018.
Haki ya kuchagua
Taarifa zisizopatikana
Mmiliki Binafsi
Kampuni
Maelezo yote
Mwaka wa kuanzishwa
Date of registration: January 17th 1994 Start: June 10th 1994
Mwanzilishi
Dr. Reginald Mengi - ni mwanaviwanda wa Tanzania, mmiliki wa vyombo vya habari na muasisi, pia ni Mwenyekiti mtendaji wa IPP Group. Pia ni Makamu wa Rais wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi Tanzania. Katika taarifa za FORBES, Mengi ni miongoni mwa mt
Mtendaji Mkuu
Joyce Mhavile - aliwahi kufanyakazi ya utangazaji katika redio na TV, IPP (ITV na Radio One). Baadae alipandishwa cheo kuwa Ofisa Mtendaji Mkuu
Mhariri Mkuu
Taarifa zisizopatikana
Mawasiliano
Independent Television (ITV)
P.O. Box 4374, Dar-Es-Salaam
Tel.: +255222775915/6
Fax: +255222775915
E-Mail: itv@ipp.co.tz
Taarifa za kifedha
Taarifa ya Kifedha
Taarifa zisizopatikana
Faida za uendeshaji
Taarifa zisizopatikana
Utangazaji(jumla ya mapato kwa asilimia)
Taarifa zisizopatikana
Isa katika soko
Taarifa zisizopatikana
Maelezo ya ziada
Taarifa ya ziada
Kiwango cha hadhira kwa mujibu wa ripoti ya viwango vya GeoPoll ya Redio & TV (Aprili – Juni 2018).