Radio Free Africa
Redio Free Africa ilianzishwa mwaka 1995 chini ya kifupisho maarufu cha RFA. Redio hii iliyopo Mwanza kwenye ziwa Victoria inatangaza kwa Kiswahili habari za kitaifa na kimataifa, burudani,, makala, matukio, maigizo, michezo na sitcoms.
Ni miongoni mwa vituo vya redio vinavyosikilizwa sana. Imekuwa kituo cha pili maarufu XX.XXX% kwa mujibu wa utafiti wa robo ya pili kuhusu hadhira ya wasikilizaji wa vituo vya redio nchini GeoPoll kwa mwaka 2018. Kituo hiki kinatangaza katika masafa 20 nchini kote. Vipindi vyake hufikia pia kanda ya Afrika Mashariki, Kati na Kusini kupitia masafa ya FM na AM.
Baada ya kituo kuanza kutangaza kwa majaribio mwezi Agosti 1995, Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) lilisita kuipa leseni ya kisheria. Kabla ya hapo, mwenyekiti Mtendaji Dkt. Anthony M. Diallo, alibaini kuwa, kimsingi, usajili ulikuwa mgumu kwa sababu tulilazimika kufuata taratibu zote za Serikali, kwa kuzingatia kuwa hata utawala wa Serikali haukuwa na uzoefu katika kipengele hiki “(barua kutoka kwa Anthony M. Diallo, Septemba 25, 1996)”.
Hivi sasa leseni ya redio ya RFA imesajiliwa kwenye Sahara Media Group Ltd (SMG) kwa 100% kwa mujibu wa Mamlaka ya MawasilianoTanzania (TCRA). SMG iliyokuwa ikiitwa Sahara Communication and Publishing Company Ltd, ilianzishwa mwaka 1992. Inaendesha vyombo vitatu vya habari vya Star TV, Redio Free Africa na Kiss FM.
Data za umiliki wa SMG hazikuweza kupatikana katika Wakala ya Usajili wa Biashara na Utoaji wa Leseni (BRELA). Kwa mujibu wa wasifu uliyounganishwa kwenye mtandao, Mwenyekiti na mtendaji mkuu wa SMG hadi sasa ni mwasisi wake Dkt. Anthony M. Diallo, alikuwa waziri katika nyadhifa mbalimbali.
Isa za hadhira
Aina ya umiliki
binafsi
Maeneo yanayofikiwa
Taifa (husikika ukanda wote wa mashariki, kati na kusini kupitia masafa ya FM na AM)
Aina ya maudhui
Maudhui huru
Kampuni ya vyombo vya Habari
Sahara Media Group Limited
Muundo wa umiliki
Radio Free Africainamilikiwa na kuendeshwa na Sahara Media Group Limited,ambayo hatimaye inamilikiwa na mwasisi wake Dr. Diallo. Hakuna data zilizopatikana BRELA
Haki ya kuchagua
Taarifa zisizopatikana
Kampuni
Maelezo yote
Mwaka wa kuanzishwa
Date of registration: September 6th 1995 Start: August 1995 on a trial basis
Mwanzilishi
Dr. Anthony M. Diallo - ni mwanasiasa na mwenyekiti wa chama wa mkoa wa Mwanza wa chama tawala cha Chama cha Mapinduzi (CCM). Alikuwa mbunge (1995 - Okt 2010) na kupoteza ubunge kwa mgombea wa upinzani. Alikuwa na nyadhifa mbalimbali katika baraza la Mawa
Mtendaji Mkuu
Anthony M. Diallo - angalia hapo juu
Mhariri Mkuu
Beatrice Rabachi - Meneja wa Vipindi. Calvin Jilala - Mhariri wa Habari.
Mawasiliano
Radio Free Africa;
Plot No. 5-7, Ilemela Industrial Area, Airport Road,
P.O Box 1732, Mwanza.
E-mail: info@radiofreeafrica.co.tz
Taarifa za kifedha
Taarifa ya Kifedha
Taarifa zisizopatikana
Faida za uendeshaji
Taarifa zisizopatikana
Utangazaji(jumla ya mapato kwa asilimia)
Taarifa zisizopatikana
Isa katika soko
Taarifa zisizopatikana
Maelezo ya ziada
Taarifa ya ziada
Kiwango cha hadhira kwa mujibu wa ripoti ya viwango vya GeoPoll ya Redio & TV (Aprili – Juni 2018).
Muhtasari wa vyombo vya habari
Research and Planning Manager, Sahara Media Group (September 2018). Media Ownership Monitor Questionnaire Sahara Media Group.