This is an automatically generated PDF version of the online resource tanzania.mom-gmr.org/en/ retrieved on 2024/03/19 at 10:45
Global Media Registry (GMR) & Media Council of Tanzania - all rights reserved, published under Creative Commons Attribution-NoDerivatives 4.0 International License.
Media Council of Tanzania LOGO
Global Media Registry

Wingi wa Hadhira

Tangu kianzishwa kwa mfumo wa demokrasia ya vyama vingi na Serikali, mwaka 1992, kumekuwa na ongezeko kubwa la vyombo vya habari na kampuni zake, Hata hivyo kuwapo na wingi tu wa vyanzo vya vyombo vya habari haina maana kuwapo na wingi wa maoni. Kwa mfano hebu angalia, kinadharia, kati ya chaneli 100 zilizopo, hadhira inaamua kutumia moja tu. Hali hii inamwachia mmiliki mmoja kuwa na ukiritimba wa kuwasilisha mawazao na maoni - na hivyo, kuwa na ushawishi mkubwa kwa maoni – na hivyo kuwa na ushawishi mkubwa kwa maoni ya umma. Hii ndiyo maana ya “Wingi wa hadhira”. 

Kiwango cha juu cha wingi hasa katika magazeti 

Nchini Tanzania hasa soko la magazeti inaonesha kiwango cha juu cha wingi wa hadhira. Tuliangali kupunguza vyombo vya juu vinne kutoka soko la magazeti linalozingatia habari. Mwananchi Communication Limited (chini ya Nation Media Group XX.XXX%) IPP media Group (XX.XXX%) New Habari (2006) Ltd. (XX.XXX%) na Tanzania Standard Newspaper linalomilikiwa na Serikali (TNS, XX.XXX%).Kampuni hizo kwa pamoja zinatoa habari zao kwenye magazeti kwa jumla ya XX.XXX%ya wasomaji. MCL inamilikiwa binafsi na kuendeshwa chini ya Nation Media Group iliyoko Kenya na kugharimiwa na The Aga Khan Development Fund. IPP Media Group Nayo ni kampuni binafsi, inayomilikiwa na mfanyabiashara maarufu aliyefanikiwa Dkt. Reginald Mengi. New Habari Limited (2006) inahisishwa na mwanasiasa na mfanyabiashara  Rostam Aziz,  hali ya kuwa wanahisa hawafahamiki, ispokuwa , baadhi ya tetesi zinaeleza kuhusiana na Aziz.

Wingi  unaeleza hali ya soko la  habari la magazeti isipokuwa magazeti ya michezo, hata hivyo vyombo vikuu ni vilevile hatakama iyaingiza magazeti ya michezo.

Soko la TV lina wingi mkubwa, kwa kuwa kampuni kuu 4, Tanzania (IPPXX.XXX%), Tanzania Broadcasting Coorporation inayomilikiwa na Serikali (TBC) XX.XXXAzam Media Limited XX.XXX% na Clouds Entertainment LimitedXX.XXX% zinawakilisha hadhira ya XX.XXX% IPP Group inamilikiwa na mjasiriamali wa vyombo vya habari, Dkt. Reginald Mengi, TBC, kwenye karatasi ni mtangazaji wa umma na kuendeshwa na Serikali kwa vitendo. (LINK kwenye Government profile). Familia ya Bakhresa inamiliki Azam Media Limited mali ya  kampuni yao kubwa ya Bakhersa Group inayoendesha biashara kuanzia vyakula hadi boti za usafiri. Joseph Kusaga, aliyeanzisha Clouds FM na kuikuza na kuendeleza, pia anamiliki hisa nyingi za kampuni, hali ya kuwa wanafamilia yake wengi wanamiliki hisa zilizobaki.

Soko la Redio:lina mambo mengi zaidi na “waongoza sko” wanatofautiana kutoka mkoa mmoja hadi mwingine. Hapa pia Clouds Entertainment LtdXX.XXX%, IPP media (XX.XXX%) na Tanzania Broadcasting Corporation (TBC): XX.XXX% inayoendeshwa na serikali, zina msimamo mzuri kwenye soko, na kila moja inaendesha vituo vingi. Sahara Media Group Ltd kutoka Mwanza yenye vituo vingi vya redio na TV, inafuatia na hadhira ya XX.XXX%. Hakuna taarifa rasmi ya kampuni kwenye masjala ya BRELA. Taarifa zinamtaja Dkt. Anthony Diallo, Mwanasiasa na mbunge wa zamani, na mwasisi, ofisa Mtendaji mkuu na mmiliki wa kampuni hiyo. Pia inawakilisha kampuni kwenye matukio ya umma. Soko la redio linaonyesha wingi wa wastani na wa kiwango cha juu kwa kuwa kampuni 4 za redio za juu zinafikia XX.XXX%ya wasikilizaji. 

Soko la mtandao: MCT iligharamia utafiti wa haraka haraka kuhusu tovuti maarufu sana. Tovuti maarufu za habari – bila ya kujumuisha mitandao ya kijamii – ni blogi huru- haihusiani na vyombo vya habari vyovyote vilivyozoeleka lakini vinaunda njia mbadala ya kutolea habari na jukwaa la majadiliano. Kuna kiwango kidogo cha wingi wa hadhira kwa vile watumiaji wanataja aina mbalimbali za habari mtandaoni. Kampuni 4 za vyombo vya habari mtandaoni zilizotajwa zilizotajwa zaidi kama vyanzo vya habari kati ya XX.XXX%ya watu waliyofanya utafiti. Wamiliki wake walianza kama waendesha blogi na wajasiliamali na kidigitali na hawaelekei kuwa na shauku ya biashara nyingine na siasa. Jamii Forum ilianzishwa na Maxence Melo na Mike Mushi, inafahamika na kutumiwa zaidi (XX.XXX%), Millard Ayo  alianzisha blogi yenye jina lake (XX.XXX%) pamoja na Ahmed Issa Michuzi  (XX.XXX%). Muungwana Blog pia ni miongoni mwa blogi zilizotajwa sana, ilianzishwa na sasa kumilikiwa na Muungwana Rashid Malik Said ambaye hajioneshi.

Sheria mpya imeweka vipingamizi vya juu zaidi vya kuingiza na hata kuwafukuza wagavi watoa huduma waliyopo watakaoshindwa kulipia ada ya usajili. 

Ukosefu wa Taarifa za Fedha – uwezo wa soko hubaki siri. 

Wakati wingi wa hadhira unahusu uwezo uliyopo kwenye kuunda maoni ya umma, wingi wa soko unaangalia nguvu ya soko ya kampuni za vyombo vya habari. Wingi wa soko maana yake ni kwamba baadhi ya kampuni za vyombo vya habari vinaweza kushawishi kiwango kikubwa cha fedha kinachotofautiana kinachoweza kupatikana kwenye sekta ya vyombo vya habari, kinachoweza kuharibu zaidi ushindani. Kiashirio cha uwezo wa fedha wa kampuni ni kiasi chake cha soko – yaani asilimia ya mapato ya kampuni moja inajipatia 99% ya fedha katika sekta itakuwa na uwezo wa kulazimisha washindani kutoka nje ya soko. Kampuni zile nyingine kwa upande wao zitakosa rasilimali kwa ajili ya kuzalisha maudhui ya ubora wa hali  juu yenye ushindani na hasa kwa ajili ya kulinda uhuru wao Ingawa ni rahisi kuchukuliwa au kushawishi wawekezaji binafsi na maslahi yao.

Nchini Tanzania kiwango cha wingi wa soko hakikuweza kubainishwa kwa sababu kwa mfano data za fedha kwenye mapato, hazipo. Mishahara midogo kwa waandishi wa habari, ugharamiaji wa fedha wa Serikali iliyoelemea upande mmoja na kuna kutoa ruzuku kwa vyombo vya habari vinavyomilikiwa na taifa, pamoja na kuongezeka mara kwa mara kwa kupungua kwa vyombo vya habari. Vipya vinavyoongezeka kila mara hasa katika magazeti inaonyesha kukosekana kwa uwiano wa kufedha kiasi cha kusindwa kufanyakazi na hata hali mbaya ya sekta ya vyombo vya habari. 

Umiliki wa vyombo vya habari Mtambuko usio samimiwa – wingi, inazidi kuongezeka. 

Wingi wa vyombo vya habari mtambuko kwa kawaida hupimwa kwa kuzingatia uwezo wa soko ambalo halikuweza kufahamika kutokana na kukosekana kwa data za fedha. Jitihada za kuanzisha kanuni ya vyombo vya habari mtambuko vinachelewa kufikia – imechelewa sana. Wakati uradua wa vyombo vya habari wameweka mada hii kwenye ajenda mapema saizi mwanzoni mwa millennia, serikali imesita. Hali hii imeruhusu kampuni za vyombo vya habari mtambuko kuzidi kupanuka. Kama vile IPP Media ltd ambavyo hivi leo ni miongoni mwa kampuni ni kubwa za vyombo vya habari katika Afrika Mahsariki inayoendesha magazeti na utangazaji na hivi karibuni imejisajili kama mtoa maudhui ya mtandao.

Kampuni hizo zinauwezo wa kuwaondoa washindani, hali ambao inahatarisha wingi wa vyombo vya habari nchini.

UPUNGUFU

Viwango vya hadhira kwa TV na Radio vinatokana  na utafiti wa GeoPoll kwa robo mwaka ya pili, 2018. Matumizi ya magazeti na mtandaoni, yanatokana na utafiti wa haraka  haraka wa GeoPoll, kwa njia ya ujumbe mfupi (arafa), uliyofanywa kwa siku mbili mwezi AAgosti / septemba. GeoPoll inaonekana kuwa shirika  linalokubalikwa, hata hivyo kimbinu, utafiti huo una upungufu wake kwa jumla, kwa mfano, unaishia wa watanzania wenye kumiliki simu za mkononi  tu – ambao mijini zaidi kuliko mtanzania wa kawaida. 

  • Project by
    Media Council of Tanzania
  •  
    Global Media Registry
  • Funded by
    BMZ