This is an automatically generated PDF version of the online resource tanzania.mom-gmr.org/en/ retrieved on 2024/03/19 at 04:24
Global Media Registry (GMR) & Media Council of Tanzania - all rights reserved, published under Creative Commons Attribution-NoDerivatives 4.0 International License.
Media Council of Tanzania LOGO
Global Media Registry

Uchumi

Tanzania inaonekana kupiga hatua kubwa kwa upande wakiuchumi kwa kuangalia wastani wa ikuaji wa mwaka wa 6% hadi 7% ya GDP katika kipindi cha miaka 15 iliyopita. Haba katika sekta za mawasiliano ya simu, huduma za fedha, biashara ya rejareja, madini utaki, ujenzi na uzalishaji zimekuwa. Ukuaji huu hata hivyo si mpana sana. Wakati GDP imekua na idadi ya watu pia nayo imeongezeka ndiyo maana idadi halisi ya watu maskini imebaki palepale gawa kiwango cha umaskini kimepungua. 

Kilimo kimeendelea kuwa uti wa mgongo wa uchumi kinachangia zaidi ya 30% ya GDP na kutoa ajira kwa takriban theluthi mbili ya idadi ya watu. 

Vyombo vya habari vinakabiliwa na hali ya wasiwasi 

Wakati hali ya uchumi kwa jumla ina mwelekeo mzuri, sekta ya vyombo vya habari inakabiliwahali ya uchumi isiyoendelevu na hivyo kuonesha mwenendo wa dunia. Serikali haifanyi jukumu kubwa kuhimiza uendelevu na uhuru wa vyombo vya habari. Baadhi ya hatua zake adimu sana ni kuondoa kodi ya ongezeko la thamani ( VAT) kwa magazeti na kamera za televisheni hata hivyo redio za jamii ndiyo pekee zinazosamehewa kodi hizo hata hivyo bado inakuwa vigumu zaidi kwao kuendesha shughuli zakekwa usahihi.

Vyombo vya habari binafsi vinaendelea peke yao, wakati mtangazaji wa umma kinadharia kupata msaada wa kifedha kupitia wizara ya habari. Mishahara ya watumishi wa TBC inalipwa moja kwa moja na wizara na bajeti zaidi inaweza kuombwa kila mwaka hata mapendekezo ya bajeti na kwa kufanya hivyo, kukwamisha shughuli za vyombo vya habari wakati mwingine serikali inashindwa hata kutoa fedha za bajeti iliyopunguzwa. Hali hii ina mwacha mtangazaji hivyo kuwa hatarini na kulazimika kuingia kwenye matangazo ya biashara. 

Changamoto katika soko la matangazo 

Soko la matangazo bado linakuwa muhimu zaidi kwa ajili ya kugharimia vyombo vya habari kwa mfano mapato ya matangazo yanagharimia takriban 85% ya gharama za uendeshaji wa magazeti. 

Serikali ina udhibiti mkubwa wa soko la watangazo:kwa mujibu wa takwimu za sheria la fedha la kimataifa (IMF) inachangia takriban 60% ya mapato ya matangazo nchini Tanzania wahariri wengi na maripata wanailaume hali katika usambazaji wa wazi wa kiwango hiki – na hivyo wavipatia vyombo vya habari vya taifa upendeleo malum na kubagua magazeti ya binafsi hasa yanayosemekana kuelemea zaidi ya binafsi kwenye upinzani kwa mfano, lilikuwa gazeti linalokosoa la mwana halisi liliondolewa kabisa kwenye matangazo ya serikali gazeti hilo bado liliendelea kuwapo kutokana na wasomaji wake wengi wa usambazaji mkubwa na liliweza kuendelea na kazi zake hata kama bila ya matangazo ya serikali. Hatua iliyofuata ilikuwa kali zaidi. Serikali imelifungia kabisa mwanahalisi kwa miaka mwili mwezi Julai 2012 na kufanya hivyo tena mwaka 2017. Mwishoe mahakama kuu ilitupilia mbali uamuzi wa Wizara wa kulifungia kwa hiyo gazeti hilo linaendelea kuchapishwa?

Kama wateja wa utangazaji kampuni za simu za mkononi na za bia za pili na tatu kwa matangazo baada ya Serikali lakini Serikali kwa ujanja kushawishi namna ya usawa ya kampuni hizo za biashara kutumia bajeti yake za matangazo kwa njia ya ubadilishanaji na hivyo kujenga mazingira mazuri yanayofaa kibiashara kwa sekta hizo kwa kutumia vyombo vya usimamizi au sheria. 

Matangazo ya serikali yameshuka kutokana na sheria ya huduma za vyombo vya habari 2016 

Tangu Rais John Magufuli alipoingia madarakani mwaka 2015, kiasi cha matangazo ya serikali kimeshuka, Sheria ya huduma za vyombo vya habari, 2016 inakataza uwekaji wa matangazo ya serikali kwa hiyo haiukupunguza upendeleo wa kisiasa wakati vyombo vya habari vya biashara vilipoanza kuangalia ujia mbadala za fedha badala ya matangazo ya serikali yamepata wanasiasa na wafanyabiashara walio tayari kufidia. Kusema kweli hatua hiyo,ina hoja na kulaumu uhuru wa uhariri kwa kiasi kikubwa. wakati huo huo vyombo vya habari vya urithi hivi sasa vinahitaji kushindana na majukwa ya matangazo, kupata sehemu ya soko la matangazo ambalo tayari limeshuka, na hivyo kusababisha changamoto nyingine za ziada na fedha kwa ajili yao. 

 

  • Project by
    Media Council of Tanzania
  •  
    Global Media Registry
  • Funded by
    BMZ